Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Septemba, 2025

DKT. BITEKO AELEZA MIAKA 10 YA MAPINDUZI YA MAENDELEO BUKOMBE

Picha
Na Mwandishi wetu  Mgombea Ubunge wa Jimbo la Bukombe kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Ndugu Doto Mashaka Biteko amesema kuwa kwa Serikali ya CCM inayoongozwa na Dkt. Samia Suluhu Hassan imefanya jitihada kubwa ya kuwaletea maendeleo wananchi wa Wilaya ya Bukombe ikiwa ni pamoja na kutoa fursa za kukuza uchumi wa Wilaya hiyo. Dkt. Biteko amesema hayo Septemba 27, 2025 wakati wa mkutano wa kampeni katika Kata ya Katente wilayani Bukombe mkoani Geita ikiwa ni sehemu Kampeni za Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani utakaofanyika Oktoba 29, mwaka huu. Amesema mwaka 2015 Kata ya Katente, Igulwa na Kata zote zilizopo maeneo ya mjini zilikuwa na kiwango duni sana cha maendeleo ikilinganishwa na maendeleo yaliyofikiwa sasa.  Amesema  Wilaya ya Bukombe ilikuwa na shule moja ya kidato cha tano na sita, hospitali moja, zahanati nne huku umeme ukiwa katika vijiji saba pekee. Amesema Serikali ya CCM imekuwa ikifanya jitihada kubwa ya  kutekeleza miradi ya maendeleo i...

KATAVI YAVUTIA MAMIA YA WATALII WA NDANI KATIKA SIKU YA UTALII DUNIANI.

Picha
Na.Happiness Sam- Katavi Mamia ya watalii wa ndani wamejitokeza leo Septemba 27, 2025 kutembelea Hifadhi ya Taifa Katavi kuadhimisha Siku ya Utalii Duniani ambayo huadhimishwa kila mwaka ifikapo tarehe hiyo kwa lengo la kutafakari na kukumbuka mchango wa sekta ya utalii katika kuchangia kipato cha mtu mmoja mmoja na dunia kwa ujumla. Akitoa hotuba wakati wa maadhisho hayo, Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko aliwapongeza TANAPA kwa kufanikisha maandalizi ya siku hiyo katika mkoa huu wenye vivutio mbalimbali vinavyouingizia mkoa mapato na ajira kwa vijana wetu. “Nitoe wito kwa wananchi wa Mkoa wa Katavi kushirikiana na TANAPA pamoja na Wizara ya Maliasili na Utalii kutunza hifadhi zetu ili ziendelee kuwa kapu la kutuingizia fedha za kigeni”, alisema Mrindoko. Kwa upande wake Naibu Kamishna wa Uhifadhi na Maendeleo ya Biashara TANAPA, Massana Mwishawa alisema katika kuenzi mchango wa utalii kwenye nyanja mbalimbali za kimais

RAIS DKT. SAMIA AMPONGEZA MWANARIADHA SIMBU

Picha
Na Mwandishi wetu  Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amempongeza Mwanariadha Alphonse Simbu kwa kuwa Bingwa wa Dunia wa mbio za marathon za Tokyo na kwamba ataendelea kutoa kipaumbele katika sekta ya michezo ili itoe mchango zaidi katika kukuza uchumi wa nchi na kuongeza wigo wa upatikanaji ajira kwa vijana   Pongezi hizo zimetolewa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo Jumamosi (Septemba 27, 2025) alipomwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwenye hafla kuwapongeza wanamichezo na timu zilizofanya vizuri kwenye medani za kimataifa, hafla hiyo imefanyika katika ukumbi wa mikutano wa hotel jijini Dar es Salaam. Katika tukio hilo Mheshimiwa Majaliwa alitangaza kuwa, Mheshimiwa Rais. Dkt. Samia amempatia Mwanariadha Simbu zawadi ya nyumba jijini Dodoma, sambamba na kikabidhiwa kitita cha shilingi milioni 20 ikiwa ni ishara ya kutambua ushindi huo ambao umeliletea Taifa heshima kwenye jukwaa la kimataifa" "Mheshimiwa Rais Dkt. Samia ameandaa nyumba iliyopo mkoani Dodoma, ambayo ita...

UN YAITAJA TANZANIA KINARA ONGEZEKO LA WATALII

Picha
Na Mwandishi Wetu TANZANIA imejumuika na mataifa mengine duniani kuadhimisha Siku ya Utalii Duniani inayofanyika Septemba 27 kila mwaka, huku imeendelea kutajwa na Shirika la Utalii Duniani kuwa miongoni mwa nchi zinazoongoza Afrika kwa ongezeko kubwa la idadi ya watalii. Akizungumza kwenye kilele cha maadhimisho hayo yaliyofanyika katika eneo la Hifadhi ya Ngorongoro (picnic site), Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Hassan Abbasi amesema ripoti ya UN Tourism ya mwaka 2024 imeitaja Tanzania kuwa kinara barani Afrika katika ongezeko la watalii baada ya janga la UVIKO-19, kwa ukuaji wa asilimia 48, ikifuatiwa na Ethiopia (40%), Morocco (35%), Kenya (11%) na Tunisia (9%). Dkt. Abbasi amesema ripoti ya mwaka huu (2025) imeionyesha Tanzania kuwa miongoni mwa nchi 20 bora duniani zinazofanya vizuri katika sekta ya utalii, kwa wastani wa ukuaji zaidi ya asilimia 50. "Idadi ya watalii wa kimataifa iliongezeka kutoka 922,692 mwaka 2021 hadi kufikia 2,141,895 mwaka 2024, sa...

ISIMILA STONE AGE YATANGAZWA MSHINDI, MKUTANO WA KIMATAIFA WA MAKUMBUSHO

Picha
Na Mwandishi wetu. Makumbusho ya Muhula wa  Zama za Mawe  Isimila (Isimila Stone Age Site Museum)  yaliyopo Mkoani Iringa nchini Tanzania yametangazwa kuwa mshindi miongoni mwa  mawasilisho bora ya urithi na utafiti wa pamoja kwenye Mkutano wa Kimataifa wa Makumbusho (ICOM 2025) unaofanyika Roma, Italia kuanzia tarehe 24-27 Septemba. Hayo yamesemwa na Mhifadhi Mambo ya Kale Mkuu kutoka  Kituo cha Nyumba  ya Kumbukizi ya Mwalimu Nyerere Magomeni, Bi. Neema Mbwana ambaye anashiriki katika mkutano huo unaofanyika Roma Italia akiambatana na Bwana  Benedict Jagadi Mhifadhi Msaidizi na Bi. Amina Salum, Mhifadhi Mwandamizi.  "Ushindi huu umepatikana baada ya andiko nililoandika kuhusu Makumbusho haya lililowasilishwa kwenye mashindano ya kitaaluma yajulikanayo kama ICOM na likachaguliwa miongoni mwa washindi" amesema Bi. Neema. Aidha,amefafanua kuwa ushindi huo unaonesha thamani ya kipekee ya Makumbusho ya Isimila kama eneo lenye zana za mawe za zaidi ya...

MRADI WA TACTIC MANISPAA YA KIBAHA KUONGEZA FURSA ZA UCHUMI KWA WANANCHI

Picha
Na Mwandishi wetu  Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA ) inatarajia kuleta manufaa makubwa kwa Manispaa ya Kibaha Mkoani Pwani na Miji mingine nchini, kupitia Mradi wa Uboreshaji Miundombinu ya Miji Tanzania (TACTIC) ukitajwa kuongeza fursa za ajira kwa Vijana na kuchochea uchumi wa Manispaa ya Kibaha chini ya Maboresho makubwa ya mazingira ya ufanyaji wa biashara yatakayofanyika. Kauli hiyo imetolewa leo Alhamisi Septemba 25, 2025 katika Soko la Mnarani, Kibaha na Mhandisi Emmanuel Manyanga, Muwakilishi wa Mtendaji Mkuu wa TARURA ambaye pia ni mratibu msaidizi wa mradi wa TACTIC wakati wa utiaji saini Mkataba wa mradi wa TACTIC kwa Manispaa ya Kibaha ukihusisha Uboreshaji wa Miundombinu ya Barabara, Soko kuu la Mnarani, Bustani ya Mapumziko na burudani pamoja na ujenzi wa Jengo la Usimamizi wa mradi ukigharimu shilingi Bilioni 19.83 bila jumuisho la kodi ya ongezeko la thamani (VAT). "Mradi huu kwa Manispaa ya Kibaha utaongeza fursa za ajira, kuchochea ukuaji wa uchu...

FAMASIA TABIBU KUCHANGIA UFANISI KATIKA HUDUMA ZA AFYA NCHINI.

Picha
Na Ngonise Kahise, Dar es salaam  Wizara ya Afya imeona tija kwa vituo vya Afya binafsi na vya Umma kuanzisha na kutekeleza  huduma ya Famasia tabibu ambayo itachangia kuongeza ufanisi katika huduma za afya. Kauli hiyo imetolewa Leo Septemba 24, 2025 Jijini Dar es salaam na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Mifupa na Ubungo Mhimbili(MOI)Dkt Mpoki  Ulisubisya katika hafla ya Sherehe ya Maadhimisho ya Wafamasia Duniani  iliyobeba  kauli mbiu isemayao" tukifikiria  Afya tufikirie na famasia  " Kauli hii imekuja katika wakati sahihi kuikumbusha Jamii ya Wafamasia juu ya jukumu kubwa lililowekwa juu ya mabega yao kuhakikisha Afya za Watanzania wote zinalindwa  wakati wote kwa kuzingatia umuhimu wa Wafamasia katika kutoa huduma kwa Wagonjwa " Amesema Mpoki Amesema wameona tija kwa Mfamasia kuwa sehemu ya  matibabu ya Mgonjwa hivyo Wizara inaendelea kuajiri Wafamasia katika huduma za Afya na kutoa ufadhili wa masomo ya ubobezi na  kutambua ubob...

UJENZI WA BARABARA ZA LAMI KUKUZA UCHUMI WA WANANCHI TANGANYIKA.

Picha
Na Mwandishi wetu.Katavi Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Mwaka 2025 Ndugu Ismail Ali Ussi, ameipongeza Wakala ya Barabara za Vijijini na Mjini (TARURA) Mkoa wa Katavi kwa kutekeleza ujenzi wa barabara za kiwango cha lami za Mji wa Majalila Wilaya ya Tanganyika Mkoani humo zenye urefu wa km 4.0 huku zikitajwa kuwa chachu ya ustawi wa maendeleo ya watu kiuchumi na Kijamii. Ussi amezungumza hayo mara baada ya kuzindua barabara hizo na kuongeza kuwa utekelezaji makini wa majukumu ya TARURA utawezesha wananchi kujikwamua kiuchumi kutokana na unafuu utakaokuwepo kutokana na kuimarika kwa miundombinu ya usafirishaji hivyo kila mmoja atanufaika na ukuaji wa uchumi. Awali akisoma taarifa kwa Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2025 Ismail Ali Ussi, Meneja wa TARURA Wilaya ya Tanganyika Mhandisi. Nolasco Kamasho amesema mradi wa barabara za Mji wa Majalila uliojengwa Kijiji cha Majalila Kata ya Tongwe una urefu wa km 4.0 na umegharimu zaidi ya shilingi bilioni 1.8...

SERIKALI YAONDOA VAT KWA VITUO VYA GESI ASILIA ILIYOSHINDILIWA (CNG)

Picha
Na Mwandishi wetu  Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Mha. Felchesmi Mramba amesema  Serikali imeondoa kodi ya ongezeko la thamani  (VAT) kwa vituo vyote vya Gesi iliyoshindiliwa (CNG) nchini  ili kuhamasisha matumizi ya gesi asilia  kwenye vyombo vya moto kupitia uwepo wa vituo vingi vya kutoa huduma hiyo kwa wananchi.  Amesema kuwa Serikali pia imeondoa kodi kwenye vifaa vya kuwekea mifumo hiyo ya gesi  kwenye vyombo vya moto kama vile magari na bajaji ikiwa ni hatua pia ya kuhamasisha matumizi ya gesi asilia katika vyombo vya moto. Mhandisi Mramba ameeleza hayo leo Septemba 24, 2025 jijini Dar es Salaam wakati  akizindua kituo cha Gesi Asilia iliyoshindiliwa (CNG) cha  kampuni ya Puma Energy kilichopo Bagamoyo road.  " Serikali inafanya jitihada hizi ili kutoa nafasi kwa watanzania kutumia gesi kwenye vyombo vyao vya moto kwa kurahisisha mazingira ya upatikanaji wake na pia kwa kuwa kuna unafuu wa gharama pale unapotumia  Gesi Asi...

TANZANIA YANG’ARA UWEKEZAJI KATIKA ELIMU KWA RASILIMALI ZA NDANI

Picha
Na Mwandishi wetu,Dar es salaam  Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema Tanzania ni miongoni mwa nchi zilizopiga hatua katika  matumizi ya rasilimali za ndani na kuwekeza katika sekta ya elimu kwa maendeleo endelevu. Amesema hayo leo Septemba 24, 2025 jijini Dar es salaam wakati akifungua Kongamano la Tano la Kimataifa la Elimu Bora lililoongozwa na kauli mbiu inayosema “Kuimarisha mifumo na uwekezaji: Kusonga mbele katika Uhamasishaji wa Rasilimali za Ndani kwa ajili ya Elimu Jumuishi, Bora na Endelevu Barani Afrika”. Dkt. Biteko ametaja hatua zilizochukuliwa na Serikali kuwa ni pamoja na kutunga na kuboresha Sera, Sheria na miongozo mbalimbali ya elimu, kuongeza kiwango cha bajeti ya elimu kutoka shilingi za trilioni 4.72 kwa mwaka wa fedha 2020/2021 hadi kufikia shilingi za trilioni 6.16   mwaka wa fedha 2024/2025. Amesema ongezeko hilo la bajeti limeboresha mazingira na miundombinu mbalimbali ya elimu kwa maendeleo endelevu. Vile vi...

RC CHALAMILA "MARUFUKU MABAUNSA KUTUMIKA KUTOA WATU MAENEO YENYE MIGOGORO DSM"

Picha
 Na Mwandishi wetu,Dar es salaam  Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe Albert Chalamila ameyasema hayo Kufuatia ukiukwaji wa sheria na vitendo vya ukatili vilivyofanywa na Mabaunsa dhidi ya wapangaji wa Bi Alice Paskali Haule kwenye nyumba yenye mgogoro iliyopo Msasani Beach jijini Dar es Salaam ambapo ameagiza kuanzia sasa mabaunsa wasitumike kutoa watu kwenye maeneo yenye migogoro badala yake madalali wa mahakama watumie jeshi la polisi ambao wanaweledi wa kufanya kazi hiyo. Mgogoro wa nyumba hiyo ambayo ni kiwanja namba 891 unahusisha mke wa marehemu Justis Lugaibula bi Alice Paskali Haule na bwana Muhamed Mustafa Yusufali ambae anaonekana alinunua nyumba hiyo kutoka kwa marehemu Justis Lugaibula enzi za uhai wake bila kumshirikisha mkewe Akizungumza jijini Dar es salaam RC Chalamila ametoa agizo hilo leo septemba 24 alipofika katika nyumba hiyo msasani beach jijini humo baada ya jana septemba 23 kuona video zikionesha mabaunsa wakitumia nguvu kubwa na ukiukwaji wa haki za bin...

TCCIA YAITAKA SERIKALI KUWEKA MIFUMO YA KISHERIA INAYOLINDA MASLAI YA WAZAWA.

Picha
  Na Ngonise Kahise,Dar es salaam  Chemba ya biashara,viwanda na kilimo Tanzania(TCCIA) imetoa wito kwa Serikali juu ya kuwepo kwa sheria na sera zitakazotoa kipaumbele kwa wazawa zaidi ili kuhakikisha ushiriki wa Watanzania katika miradi mikubwa ya kiuchumi umekuwa wa dhati na wenye tija zaidi. ‎Akizungumza leo Septemba 23,2025 katika mkutano na Waandishi wa Habari kwenye makao makuu ya Ofisi zao,Gerezani Jijini Dar es salaam Rais wa TCCIA Vincent Minja alieleza wakati sahihi umefika kwa taifa kuwa na sera na sheria mahsus zinazolenga kuwawezesha wananchi kiuchumi. ‎ ‎" Tunaipongeza Serikali kwa kuwavutia wawekezaji wa ndani na nje lakini bado tunakabiliwa na changamoto ya ushiriki mdogo wa Watanzania katika miradi ya kimkakati hivyo ni muhimu sasa kuweka mifumo ya kisheria inayolinda maslai ya wazawa",amesema Minja. ‎ ‎Minja amebainisha kuwa sheria zilizopo zina msingi mzuri lakini zinahitaji marekebisho kwa mfano sheria ya Local Content na sheria ya Ununuzi wa Umma(PP...

MKUU WA MKOA WA DAR ES SALAAM AWAKABIDHI WAKUU WA WILAYA NA GOLIKIPA WA TAIFA STARS MAGARI YA KIFAHARI.

Picha
Na Ngonise Kahise,Dar es salaam   Serikali yawakabidhi magari mawili kwa Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Albert Msando na Mkuu wa Kigamboni lengo  likiwa ni kutumika kama chombo cha kwenda kutatua matatizo ya Watanzania. ‎ ‎ ‎Akizungumza katika hafla fupi ya makabidhiano ya Magari hayo leo Septemba 22,2025 mbele waandishi wa habari pamoja na viongozi mbalimbali katika ofisi za halmashauri ya kinondoni, Jijini Dar es salaam Mkuu wa Mkoa Albert Chalamila ametoa Shukrani kwa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu kwa kufanikisha kwani wakuu wa Wilaya walikuwa na Magari chakavu. ‎ ‎Pia ameongeza kuwa magari hayo yakatumike kuleta umoja kati ya wananchi na Serikali. ‎ ‎Vilevile Chalamila amekabidhi gari kwa golikipa wa timu ya taifa Yakub Seleman Ally kwa kufanikisha kulinda magoli mengi katika mashindano ya Chan katika mechi ya  Taifa stars na Morocco. ‎ ‎"Kama mnakumbuka vizuri tuliwahi kuhaidi kwamba yale mashindano ya michuano ya Chan kati ya Tanzania na Morroc...

CHINI YA UONGOZI WA RAIS SAMIA VIWANDA VYA SUKARI VYAIMARISHWA NA KUBORESHWA

  Na Mwandishi wetu  Chini ya Rais Samia Serikali imeendelea na utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Kiwanda cha Sukari Mkulazi kwa kuhakikisha kuwa kiwanda kinafanya kazi kikamilifu, kinatoa ajira na kinachangia katika uchumi wa taifa. Aidha uzalishaji wa sukari ulianza mwezi Julai, 2024, na kimezalisha tani 19,124 za sukari ya majumbani vile vile kimetoa ajira za moja kwa moja 2,172 na zisizo za moja kwa moja 8,000.  Kwa mujibu wa hotuba ya bajeti ya wizara ya viwanda na biashara ya mwaka 2025/26; Serikali pia imefanya upanuzi unaohusisha usimikaji wa mitambo yenye uwezo mkubwa wa kuzalisha sukari na inayotumia teknolojia ya kisasa katika kiwanda cha Sukari cha Kilombero na Kiwanda cha Sukari cha Kagera.  Katika Kiwanda cha Kilombero upanuzi unatarajiwa kuongeza uzalishaji wa 80 sukari kutoka tani 132,000 za sasa hadi tani 271,000 za sukari ifikapo mwaka 2025/2026 na kutoa ajira 4,634.  Aidha, upanuzi huo utagharimu zaidi ya shilingi bilioni 570 hadi utakapokamil...

MAKAMU WA RAIS AHUTUBIA MKUTANO WA KAMATI YA KITUO CHA KUDHIBITI MAGONJWA AFRIKA (CDC)

Picha
  Na Mwandishi wetu  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango amesema Tanzania inasisitiza umuhimu wa mifumo endelevu ya ufadhili ili kuhakikisha uthabiti wa kukabiliana na dharura za afya ya umma barani Afrika. Makamu wa Rais amesema hayo wakati akishiriki katika Mkutano wa Kamati ya Wakuu wa Nchi na Serikali wa Kituo cha Kuzuia na Kudhibiti Magonjwa Afrika (CDC) uliyofanyika pembezoni mwa Kikao cha 80 cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa Jijini New York nchini Marekani. Amesema Tanzania imedhamiria kuongeza ukusanyaji wa rasilimali za ndani, kuimarisha masuluhisho ya kibunifu ya ufadhili pamoja na kuunga mkono mipango ya kikanda ambayo inapunguza utegemezi wa misaada kutoka nje, na hivyo kuhakikisha kuwa vipaumbele vya afya vya Afrika vinashughulikiwa na serikali za Afrika.   Aidha, Makamu wa Rais amesema uzalishaji wa ndani wa vifaa vya uchunguzi, matibabu, na bidhaa nyingine muhimu za matibabu ni muhimu katika kujitegemea kweye sekta ya ...

EU YATOA TAHADHARI KUHUSU KUPUNGUA KWA BARAFU MLIMA KILIMANJARO.

Picha
 *EU YATOA TAHADHARI KUHUSU KUPUNGUA KWA BARAFU  MLIMA KILIMANJARO.* Na. Mwandishi wetu - Kilimanjaro. Umoja wa Ulaya (EU) umetahadharisha kuhusu kasi ya kupungua kwa barafu katika Mlima Kilimanjaro, hatua inayotajwa kuathiri kwa kiasi kikubwa mazingira na maisha ya jamii zinazotegemea rasilimali za mlima huo. Akizungumza jana Septemba 19, 2025 wakati wa ziara ya Waheshimiwa mabalozi wa Umoja wa Ulaya waliotembelea Hifadhi ya Taifa ya Kilimanjaro, Balozi wa Finland Nchini Tanzania. Mhe. Theresa Zitting amesema hali ya kuyeyuka kwa barafu katika kilele cha Uhuru ni ishara ya wazi ya mabadiliko ya tabianchi yanayoikumba dunia. “Ni jambo la kusikitisha kusikia na kushuhudia jinsi barafu inavyopungua na namna hali hiyo inavyotarajiwa kuathiri mtiririko wa maji na mfumo wa ikolojia katika maeneo ya chini ya mlima. Tatizo hili halipo Tanzania pekee; hata nchini mwangu Finland tunashuhudia mabadiliko ya joto,” alisema. Kwa mujibu wa takwimu zilizotolewa, takribani watalii 60,000 hute...