Machapisho

MAJALIWA ASHIRIKI SHEREHE ZA KUAPISHWA RAIS HERMINIE WA JAMHURI YA SHELISHELI

Picha
Na Mwandishi wetu  WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameungana na viongozi wa nchi za India, China, Mauritius na Comoro kwenye sherehe za kumuapisha Rais wa Jamhuri ya Shelisheli, Dkt. Patrick Herminie zilizofanyika kwenye Uwanja wa Umoja, jijini Victoria nchini humo. Waziri Mkuu ambaye amemwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, alikuwa miongoni mwa viongozi hao wakuu wakiwemo Makamu wa Rais, Mawaziri Wakuu na viongozi wa juu kutoka vyama rafiki vya siasa. Rais Herminie aliapishwa jana (Jumapili, Oktoba 26, 2025) kuwa Rais wa sita wa nchi hiyo. Viongozi hao ni Makamu wa Rais wa India, Bw. Chandrapuram Ponnusamy Radhakrishnan; Waziri Mkuu wa Mauritius, Dkt. Navinchandra Ramgoolam; Makamu wa Rais wa Chama cha Chinese People’s Political Consultative Conference (CPPCC) Bw. Gao Yunlong na Rais wa Baraza la Mawaziri la Kamisheni ya Bahari ya Hindi ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Nje wa Comoro, Bw. Mohamed Mbae. Mheshimiwa Waziri Mkuu ameambatana na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikian...

ELIMU YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA YAWAFIKIA MAAFISA DAWATI NGAZI YA MIKOA NA HALMASHAURI

Picha
 Na Mwandishi wetu  Wizara ya Nishati imeanza kutoa elimu kuhusu Nishati Safi ya Kupikia kwa Maafisa Dawati wa Nishati Safi ya Kupikia ngazi ya mikoa na halmashauri kwa lengo la kuwa na uelewa wa pamoja katika utekelezaji wa Mkakati wa Taifa wa Nishati Safi ya Kupikia pamoja na kuwawezesha Maafisa Dawati kutambua majukumu yao katika utekelezaji wa mkakati.. Akifungua mafunzo hayo, wilayani Kibaha mkoani Pwani, Mwakilishi wa Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani, Bi. Hadija Mruma ameipongeza Wizara ya Nishati kwa jitihada mbalimbali inazochukua kwa vitendo katika kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia nchini mojawapo ikiwa ni kuhakikisha elimu na vifaa vya nishati safi ya kupikia vinafika hadi ngazi za Mikoa, Halmashauri na Vijiji. Ameeleza kuwa Mkoa wa Pwani unachukua hatua mbalimbali kuhakikisha kuwa wanachi wanatumia nishati safi ya kupikia katika ngazi ya taasisi, kaya n.k akitoa mfano kuwa asilimia 76 ya taasisi zinazolisha watu zaidi ya 100 mkoani humo zimeshaham...

SERIKALI ILIVYOBADILI SURA YA AJIRA NA MASLAI YA WATUMISHI WA UMMA.

Picha
Na Mwandishi wetu  KATIKA kipindi cha miaka minne ya Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan, sekta ya utumishi wa umma imepiga hatua katika kuboresha maslahi, ustawi na mazingira ya kazi ya watumishi wa umma nchini. Kwa mujibu wa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, George Simbachawene, serikali imeweka msukumo maalum kuhakikisha watumishi wanathaminiwa, wanalindwa na wanapata haki zao kwa wakati. MASLAHI YABORESHWA Waziri Simbachawene anasema Rais Samia amefanya mageuzi makubwa katika eneo la maslahi ya watumishi wa umma. Miongoni mwa hatua hizo ni kupunguza Kodi ya Mshahara (PAYE) kutoka asilimia tisa hadi nane, na kuongeza kiwango cha chini kinachotozwa kodi kutoka Sh. 170,000 hadi Sh. 270,000. Hatua hiyo imewezesha serikali kuwasamehe watumishi kodi yenye thamani ya Sh. bilioni 14.78. Vilevile, Waziri Simbachawene anasema serikali imefuta tozo ya asilimia sita (retention fee) iliyokuwa ikikatwa kwa watumishi walio...

JEMA AFRICA WAZINDUA MFUMO WA ZABUNI WA UNUNUZI WA MAGARI WA MOJA KWA MOJA MTANDAONI ‎

Picha
Na Mwandishi wetu  Kampuni ya Jema Africa imezindua Mfumo wa zabuni wa Ununuzi wa magari moja kwa moja mtandaoni iitwayo Online vehicle Live Bidding System ikiwa ni mara ya kwanza kwa mfumo huu kutumika nchini Tanzania na ukanda wote wa Afrika Akizungumza katika uzinduzi huo uliofanyika jijini Dar es Salaam, Mkuu wa Kitengo cha Kampuni ya JEMA AUTO, Bw. Lazaro Lutobeka, alisema mfumo huo ni hatua muhimu katika mageuzi ya kidigitali yanayolenga kurahisisha upatikanaji wa magari moja kwa moja kutoka Japan kwa uwazi, uharaka na gharama nafuu. “Mfumo huu wa mnada wa magari mtandaoni ni wa kwanza wa aina yake nchini. Unamwezesha mnunuzi kushiriki moja kwa moja kwenye mnada halisi wa magari unaofanyika Japan kwa wakati huo huo, bila haja ya kusafiri. Ni mageuzi makubwa yanayolenga kuongeza ufanisi, uwazi na ushindani wa haki kwa wateja wetu,” alisema Bw. Lutobeka. Kwa mujibu wa Bw. Lutobeka, mfumo huu umeunganishwa na zaidi ya minada mikubwa 40 ya magari nchini Japan, na kupitia tovuti y...

WAZIRI WA MAMBO YA NJE AZINDUA MKUTANO WA TCCIA

Picha
  Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo, amezindua Mkutano Mkuu Maalum wa Chemba ya Biashara, Viwanda na Kilimo Tanzania (TCCIA) jijini Dar es Salaam, ambapo amesisitiza umuhimu wa taasisi hiyo kuwa injini kuu ya kuimarisha diplomasia ya uchumi nchini.  Mhe. Kombo amesema licha ya mchango wake mkubwa katika kukuza biashara, TCCIA imepoteza fursa muhimu za kimataifa, hivyo ni wakati muafaka kwa taasis hiyo kujipanga upya ili kuwa daraja madhubuti kati ya sekta binafsi na Serikali kwa kuvutia uwekezaji, kutengeneza ushirikiano wa kimataifa, kukuza masoko ya bidhaa nje ya nchi na kuhamasisha matumizi ya teknolojia za kisasa.  Aidha, ameitaka TCCIA kuwa mshauri wa Serikali katika kukuza biashara za kimataifa, kuongoza safari za wafanyabiashara nje ya nchi, na kutoa taarifa sahihi za masoko ya kimataifa. Amesisitiza kuwa Wizara itaendelea kushirikiana kwa karibu na TCCIA kupitia jukwaa la diplomasia ya uchumi ili kuiunganis...

TAASISI ISIYO YA KISERIKALI CIP YATOA TATHMINI YA KURA ZA MAONI YA UCHAGUZI MKUU.

Picha
 Na Mwandishi wetu Takwimu zinaonyesha Asilimia 83 ya Wananchi walioshiriki Kura ya maoni kutoka Mikoa 19 wamethibitisha kushiriki Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa Kufanyika Oktoba 29,2025 kwa kupiga Kura Takwimu hizo zimetolewa na Kituo cha Sera za Kimataifa-Afrika(Centre for International Policy -Afrika CIP-Africa) ambapo kuanzia 30 Septemba hadi Oktoba 5,2025 waliendesha zoezi kura za maoni Kuhusu Uchaguzi Mkuu wa Rais,Wabunge na Madiwani ili kupata twaswira ya hisia za Wananchi Kuhusu Hali ya kisiasa na mwelekeo wa Uchaguzi wa nafasi za wagombea Kupitia vyama vyao. Akizungumza na Waandishi wa habari leo Oktoba 22,2025 Jijini Dar es salaam Mkurugenzi wa Tafiti na Uchapishaji wa CIP, Thabit Mlangi amesema wamefanya zoezi la kukusanya Kura za maoni kutoka katika Mikoa 19 Tanzania Bara huku Zanzibari Ikiwa miwili Pemba na Unguja ambapo Jumla ya waliohojiwa ni 1,976, wanawake walikuwa 988 na wanaume 988 Kati ya 1,976 waliohojiwa  "Asilimia 29 walikuwa na umri kati ya miaka 18 hadi...

DKT.NCHIMBI AOMBA KURA DODOMA MJINI, KESHO KUANZA KAMPENI MOROGORO.

Picha
Na Mwandishi wetu  MGOMBEA Mwenza  wa urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Emmanuel John Nchimbi, amesema miongoni mwa mipango ya chama hicho kwa miaka mitano ijayo kikirudi tena madarakani ni kujenga Maktaba ya Taifa mkoani Dodoma. Dkt. Nchimbi ameyasema hayo leo Oktoba 17, 2025, katika mkutano wake wa hadhara wa kampeni za CCM uliofanyika Wilaya ya Dodoma Mjini alipokuwa akimuombea kura mgombea urais wa chama chake Dkt. Samia Suluhu Hassan pamoja na wagombea ubunge na udiwani ikiwa zimesalia siku 12 kabla ya uchaguzi mkuu wa Oktoba 29, 2025. “Maktaba hiyo itahifadhi kumbukumbu, nyaraka na maandiko mbalimbali ya kitaifa, na itatumiwa na watafiti, wanafunzi na wananchi kwa ujumla kwa maslahi ya taifa.” Aidha Dkt.Nchimbi ameeleza kuwa Serikali ya  CCM pia imedhamiria kujenga shule mpya za msingi 21 na sekondari 16, madarasa 150, maabara 15 za sayansi na mabweni 17 ili kuboresha mazingira ya elimu na kupunguza msongamano darasani. Hata hivyo baada ya kufanya mkutan...