Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Novemba, 2025

DKT ROGERS SHEMWELEKWA AFANYA ZIARA YA KIKAZI KATA YA PICHA YA NDEGE

Picha
Mkurugenzi wa Manispaa ya Kibaha, Dkt. Rogers Shemwelekwa, akiwa ameambatana na Wakuu wa Divisheni na Vitengo mbalimbali, amefanya ziara ya kikazi katika Kata ya Picha ya Ndege yenye lengo lakutembelea na kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo inayoendelea katika kata hiyo. Katika ziara hiyo, Dkt. Shemwelekwa ametembelea miradi ya uchongaji barabara(milioni 30 mapato ya ndani) ujenzi wa vituo vya kibiashara kwa mbonde ( milioni 562.5 mapato ya ndani) , pamoja na ukamilishaji wa chumba kimoja cha darasa katika Shule ya Msingi Lulanzi ( milioni 8 mapato ya ndani). Aidha, amekagua maendeleo ya ujenzi wa majengo ya Hospitali ya Wilaya ( Milioni 706.7 mapato ya ndani na Serikali kuu, Ununuzi wa Vifaa tiba,( milioni 300 Serikali kuu) , Ofisi ya Kata ya Picha ya Ndege ( milioni 24.5 mapato ya ndani)na ujenzi wa chumban kimoja Cha darasa shule ya msingi Mkuza (milioni 20 mapato ya ndani) Vilevile, Mkurugenzi huyo alifanya mkutano wa hadhara uliolenga kusikiliza na kutatua kero mbalimbali ...

TLS KUTOA HUDUMA ZA UTETEZI BILA MALIPO KWA WANAOTUHUMIWA KUFANYA VURUGU KIPINDI CHA UCHAGUZI

Picha
Chama cha mawakili Tanganyika (TLS) wametoa  msaada wa kisheria bila malipo wala masharti yeyote kwa watuhumiwa wote waliofikishwa  na watakaoendelea kufikishwa mahakamani  katika  mikoa mbalimbali nchini Tanzania baada ya Uchaguzi mkuu ili kuwawakilisha makahamani,kuwatembelea magerezani na kwenye vituo vya Polisi  ‎ ‎Akizungumza leo 11 Novemba 2025 na waandishi wa habari Posta Jijini Dar es salaam Wakili wa Mahakama kuu Maduhu William amesema kuwa Tarehe 7 Novemba walianza kuona watuhumiwa  mbalimbali wakifikishwa mahakamani kwa makosa ya uhaini,unyang'anyi wa kutumia silaha,uharibifu wa mali,kufanya fujo na makosa ya kula njama. ‎ ‎"Jumla ya Watuhumiwa wa makosa hayo ni 641 mpaka leo wamekwisha fikishwa katika mahakama mbalimbali kote nchini na makosa takribani yote hayana dhamana na kwa mujibu wa sheria ya nchi yetu uhaini na na makosa mengine hayadhaminiki hivyo baada ya mashtaka kusomwa mahakamani Watuhumiwa wote walipelekwa mahabusu na adhabu ya juu ...